Site Loader

Tumbo/Matumbo

Unaweza kupoteza ladha ya kula katika uwanda wa juu na  magonjwa  yake huweza kukufanya uhisi mgonjwa.kubadili vyakula huweza pia kuathiri hamu yako ya kula au kuharisha

Ziara nyingi za nyanda za juu ziko kwenye maeneo ambapo pana shida na usafi wa maji ,kwa hiyo hatari ya mharo ni kubwa.Heri nusu shari kuliko shari kamili.Maji ya makopo na machujio ya maji yaweza kutoaminika.Madini joto ndiyo dawa isipokuwa ukiwa na ugonjwa wa tezi la shingo au ujauzito.

Endapo unaharisha epuka kupungua kwa maji mwilini kwa kunywa maji mengi yaliyo safi na salama au unywe dawa ya kuongeza maji.kuna uwezekano kwa mharo wa wasafiri kusababishwa na bakteria hivyo ni vema kutumia antibayotiki.

Kama una tatizo la mmng’enyo wa chakula au kuvimbiwa nyumbani,muone daktari kabla ya safari.Kuvimbiwa kunaweza kuwa janga pamoja na mmeng’enyo hovyo kwenye nyanda za juu.Epuka mmeng’enyo mbaya unaosababisha dawa za maumivu.Unywaji wa maziwa,mtindi,huweza kupunguza tatizo.

Karatasi za chooni zilizooza, vinyesi huharibu mazingira.Siyo tu uyaache!

Usisahau kunawa mikono.

Kwenye uwanda wa juu:
• Kunywa maji mengi.
• Chukua vitafunwa uvipendavyo kwa ajili ya kula pale ambapo hujisikii kula vyakula vingine.
• Osha mikono kila mara.

Maandalizi:
• Panga namna ya kupata maji safi na salama ili usiogope kunywa mengi.
• Uwe na kikoba chenye unga wa kuongeza maji na madini mwilini na ujue namna ya kuutengeneza.
• Chunguza chanzo cha mharo wa msafiri na namna ya kuutibu.
• Muwe na mpango wa wanamsafara wa jinsi ya kutunza karatasi za chooni

Akiwa juu kabisa ya ukanda wa barafu ya kusini kabisa mwa Amerika,Argentina na Chile ielekeayo milima ya Andesi kuelekea bahari ya Antlanktiki,maarufu kama barafu ya Patagonia,mpanda mlima aliamrisha kusimama ili atoe nguo za kutelezea kwenye barafu akiwa kwenye kamba kwa sababu ya mharo wake.Akiwa kambini usiku ule,alimeza dawa za antibayotiki na aliweza kuendelea siku iliyofuata

Previous         Next